SAA YA MUUJIZA WAKO NI SASA!
Mojawapo ya nguzo zinazolisimamisha kanisa la Maranatha Reconciliation na makanisa mengine ya watu wa Mungu, ni maombezi. Maombezi, ndiyo yanayolifanya kanisa la Kristo, liendelee kudumu katika kuyafanya mapenzi ya Mungu. Huduma hii ya maombezi katika makanisa ya Upatanisho ya Maranatha, iko wazi kwa mtu yeyote anayehitaji msaada kutoka kwa Mungu. Maombi katika idara hii, huendeshwa na watu wanaoupenda mwili wa Kristo na waliojiweka wakfu kwa ajili ya huduma hii. Kwa kuwa maombezi yanahusika na siri za watu, maombi yote yanayopokelewa katika idara hii, hushughulikiwa kwa siri bila kutolewa kwa mtu yeyote. Hali kadhalika, baada ya maombi kujibiwa, majibu hayatatangazwa kwa mtu yeyote hadi pale mhusika, atakapotoa kibali. Uwajibikaji huu katika kuomba na kutunza siri za watu, ndio unaoifanya idara hii kukimbiliwa na maelfu ya watu ndani na nje ya Tanzania, wanaohitaji kupelekwa mbele za kiti cha enzi cha Mungu. Kama wewe ni miongoni mwa wale wanaolia usiku na mchana kutokana na mwiba unaoyasonga maisha yako au ya familia yako, iletee timu hii ya maombi mahitaji yako. Unaweza kufanya hivyo kwa kujaza fomu ya maombi na kuituma kwetu kwa njia ya barua pepe, fax, simu au posta. |
|
|---|---|
Kuhusu Huduma
- Sisi ni nani?
- Nini tunachokifanya
- Ndani ya Kanisa la Maranatha
- Umisheni: Tanzania & Africa
- Maoni yako
AGIZA JARIDA LA
NG'ANG'ANIA BURE
|
![]() |
-
Usoma Shuhuda za matendo makuu ya Mungu. Makala za neno la Mungu pamoja na mafundisho ya Askofu Rodrick Mbwambo bila kusahahu mafundisho yenye nguvu na Mch. Belobaba wa Marekani.
Na Habari mbalimbali utazipata ndani ya jarida la Ng'ang'ania














