Kwa mara nyingine tena kanisa la Maranatha Reconciliation Church linakuletea semina kubwa ya kitaifa ya kila mwaka itakayofanyika kuanzia tarehe 10 Oktoba hadi 16 Oktoba, 2011, kwenye makao makuu ya kanisa jijini Dar es Salaam.
Katika semina hii ya ajabu, mhubiri wa kimataifa ndugu Ben Hanegraaff kutoka Uholanzi atakuwepo kuhudumu neno la Mungu. Hali kadhalika wahubiri kutoka Kenya watafundisha neno la Mungu wakishirikiana na baadhi ya walimu kutoka Tanzania.
Mtumishi wa Mungu Ben Hanegraaff anatarajiwa kuwasili nchini tarehe 30 Septemba, 2011 ambapo yeye pamoja na mwenyeji wake Askofu Rodrick Mbwambo wataanza safari ya semina hii mikoani, Tanzania Bara, kabla ya kumalizia jijini Dar es Salaam.
Pamoja na vipindi vya neno la Mungu visivyopungua vitano kwa siku, ambapo kipindi kimoja kitakuwa kikifanyika usiku, pia kutakuwa na warsha za aina mbalimbali kama vile Ujasiriamali, Akina Mama, Vijana, n.k.
Inatarajiwa katika semina hii kuwepo kwa uimbaji usio wa kawaida wa sifa na kuabudu, kwaya pamoja na waimbaji binafsi ambao kwa pamoja watamwimbia Bwana na kuuvuta uwepo wa Mungu wakati wa semina.
Wanasemina wasiopungua mia mbili wanatarajiwa kuhudhuria semina hii wakitokea mikoani, ambao wataweka kambi kwenye makao makuu ya kanisa. Kwa wanasemina wanaotokea Dar es Salaam hawatapewa malazi, isipokuwa chakula cha mchana tu. Hadi sasa maandalizi yanaendelea vizuri kwa neema ya Mungu.
Huduma ya chakula na vinywaji kama kawaida itatolewa kwa ubora zaidi tofauti na ilivyokuwa katika semina ya mwaka jana.
Askofu Rodrick Mbwambo pamoja na mkewe Grace Mbwambo wanapenda kukualika katika semina hii ya kipekee bila kukosa. Usikose, na mweleze na mwingine. Habari zaidi utaendelea kuzipata pia kupitia
![]() |
![]() |
|---|
Pia unaweza kutufuatilia kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter |
![]() |
![]() |
|---|
![]() |
|---|
| SIFA NA KUABUDU |



















